Thursday, 11 August 2016

ZIJUE NCHI ZILIZO KWAPUA MEDALI NYINGI MPAKA SASA KTK OLIMPIK

 nintchdbpict000258060836


Mpaka sasa michezo hiyo imekwishafanyika kwa kiwango kikubwa na hivyo kupata Orodha ya timu zinazoongoza mpaka sasa katika kunyakuwa medali nyingi kwa upande wa Dhahabu, Shaba pamoja na Fedha huku jumla ya mataifa 206 yanashiriki Olimpiki ya mwaka huu.
Marekani ni nchi kinara katika medali hizo, huku ikiwa na jumla ya medali 22 kwa kujumuisha michezo yote na mpaka kufikia sasa, akijinyakulia medali 6 za dhahabu, 8 za shaba pamoja na medali 8 za Fedha.
Nchi inayofuatia ni China wakiwa na medali 16 mpaka sasa wakiwa na medali 7 za dhahabu medali 3 za shaba pamoja na medali 6 za fedha, kwa hiyo China kuwa nchi ya kwanza kwa kuwa na medali nyingi za Dhahabu akifuatiwa na Marekani ikifuatiwa na Australia.
Nchi zingine ni pamoja na Australia mwenye medali 8 mpaka sasa huku akiwa na medali 4 za dhahabu 4 za Fedha na kuambulia patupu katika medali ya Shaba.
Kiujumla katika medali zote Urusi imeshikilia nafasi ya nne kwa jumla ya medali 12, Japani 12 huku ikifuatiwa na Italia medali 9, Korea Kusini medali 6 pamoja na Ufaransa 6, Canad 5, huku Hungary pamoja na Thailand zikiwa na medali 4.
Ujerumani pamoja na Taipei ya China zote zina medali 3, huku wenyeji Brazil, Ubelgiji, Ugiriki, Uholanzi, Sweden zote zikiwa na medali mbli kila moja, na nchi pekee kutoka Afrika, Afrika Kusini ikiwa na jumla ya medali mbili amabzo zote ni za Fedha moja ikipatikana katika kuogelea walizoshinda Cameron Van De Burgh pamoja na Chad Le Clos

No comments:

Post a Comment